Matembezi ya hisani - Segerea, sehemu ya 1
Jumamosi, tarehe 22 IX 2007 Matembezi ya Hisani yaliongozwa na Mwadhama Cardinali Policarp Pengo katika parokia ya Roho Mtakatifu Segerea-Dar es Salaam.
Madhumuni ya matembezi ni kuchangia ujenzi wa kanisa la Segerea awamu ya tatu. Matembezi yalianzishwa kwenye Eneo la Seminari Kuu-Segerea na yalimalizika mbele ya kanisa jipya.
Baadaye Card. Policarp Pengo aliongoza ibada fupi ya kumshukuru Mungu kwa ujenzi halafu mnada imefanika. Tunamshukuru Mungu kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana.
Uangalie picha za Matembezi Haya.
